1. CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AGUSTINO, TANZANIA
KITUO CHA BUKOBA
KITIVO CHA ELIMU
IDARA : KISWAHILI.
JINA LA KOZI: MOFOLOJIA YA KISWAHILI.
MSIMBO WA KOZI: SW 224
JINA LA MHADHIRI: LUPAPULA, ABEL.
JINA LA MWANAFUNZI: MAPESA, NESTORY
NAMBA YA USAJILI : BAEDII 41584
AINA YA KAZI: KAZI BINAFSI.
TAREHE YA UWASILISHAJI: 28/03/2014
Swali;
Unyambuzi na Uambatizi ni dhana telezi. Jadili
2. Rubanza (1996:98) Unyambuaji kama ulivyo uambishaji unahusu upachikaji wa mofimu
katika mofimu mzizi aidha unahusu upachikaji wa mofimu zinazofuata mzizi yaani mofimu
fuatishi.
Matinde ( 2012:119) Unyambulishaji ni mbinu ya uuundaji wa maneno hivi kwamba
viambishi mbalimbali huambikwa kwenye mzizi husika ili kuunda neno jipya.
Massamba na wenzake ( 2009) Uambishaji katika lugha ni uwekaji pamoja na viambishi
na mzizi kwa namna mbalimbali bila kutilia maanani suala la aina ya maumbo yanayopatikana
alimradi tu miunganiko inayotolewa ikubalike kisarufi katika lugha, uambishaji kisarufi ndio
wengine wanauita uambatizi.
Rubanza (1996:90) Uambatizi ameuita kuwa ndio uambishaji ambao ni upachikaji wa
mofimu katika mzizi ambao huonesha upatanisho wa kisarufi wa vipashio vingine vya sentensi.
Habwe na Karanja (2004) anasema uambishaji ambao wengine huuita uambatizi ni
utaratibu wa kuongeza viambishi katika mofimu mzizi wa neno wanasema viambishi huweza
kuambikwa kabla, katikati na baada ya mzizi wa neno.
TUKI ( 2009:89) Uambishaji katika taaluma ya mofolojia huu ni utaratibu wa kuweka
kiambishi, kabla, katikati au baada ya mzizi.
UTELEZI WA UAMBATIZI NA UNYAMBUZI
Ni ukweli kwamba unyambuzi na uambatizi ni dhana telezi kwani kumekuwapo na
mikanganyiko juu ya dhana hizi mbili kulingana na wataalamu mbalimbali katika kuelezea,
kwa mujibu wa Rubanza amechanganya dhana mbili tofauti yaani uambatizi na Uambishaji
kuwa ni kitu kimoja. Rubanza ameeleza kuwa Unyambulishaji unagawanyika sehemu mbili
ambazo ni Uambishaji na Unyambuaji Vilevile kwa kuwarejelea Habwe na Karanja pamoja na
TUKI (2009) wao wanatoa dhana ya Uambishaji pekee na wanashindwa kutoa dhana kamili ya
Uambatizi hivyo kuzifanya dhana hizi kuendelea kuwa na mikanganyiko na kuwa telezi. Vile
vile kuna wataalamu mbalimbali bado wanakinzana katika kuelezea dhana hizi.
Kutokana na maelezo yao ninaweza kuthibitisha uambishaji ndio umegawanyika sehemu
mbili ambazo ni Uambatizi na Unyambuzi, hivyo usahihi wa fasili za dhana hizi ni kuwa;
Uambatizi ni mchakato unaohusu upachikaji wa viambishi tangulizi mwanzoni mwa
mzizi wa neno ili kulipa nen hilo maana maalumu yaaani upatanisho wa kisarufi.
Unyambuzi ni uwekaji viambishi fuatishi kwenye mzizi wa neno na tokeo lake ni
kubadili aina ya neno mfano; msomi kutokana na kitenzi soma hivyo kile kinacholeta tofauti ni
kinyambuzi na ni sharti kila nomino ziwe katika ngeli kwani nomino zenye sifa sifa moja
zinazofanana huwekwa pamoja.Kila kinyambuzi kina maana yake.
3. fasili za dhana hizi mbili wapo wengine wanaochanganya dhana ya Uambishaji kuwa ni sawa na
uambatizi kama alivyoeleza Rubanza na TUKI
Kuna michakato au mifanyiko ya uambatizi kama vile;
Nafsi; Nafsi hutazamwa kama kiima nafsi I, II na III ambapo katika tungo nafsi imegawanyika
katika pande mbili yaani kiima kinaweza kuwa na viambishi kama ,ni-, -u-, -a-, -tu-, -m-,-wa-
mfano; mtoto, utoto. Yambwa inaweza kuwa na viambishi kama vile ni- ku- m- tu- wa- ji –ni
Ukanushi; katika ukanushi kuna viambishi kama vile ha----i, si----i mfano; hawalimi, sitaki
Uhali; uambatizi wenye kuonesha uhali viambishi vyake ni kama vile po- ki- nge- ngali- ka- li-
mfano; walipokula, Angekuja
Unjeo; mchakato huu huonesha wakati tendo limetendeka. Katika mchakato huu viambishi vya
vipo katika uyakinishi kama vile –li-, me-,-na, -ta-, mfano; Anakula, amekula, alikula atakula.
Kiambishi na kinaonesha wakati uliopo, me inadokeza wakati uliopo katika hali timilifu li
inadokeza wakati uliopita na ta wakati ujao. Vilevile kuna njeo inayodokeza ukanushi kama ku-
ja i ta
Idadi na wingi (viambishi ngeli): mchakato huu unaonesha makundi ya nomino yaani ngeli
kama vile m-wa, ki- vi. Uambatizi huweza kufanyika katika aina mbalimbali za maneno kama
ifuatavyo;
Uambatizi huleta upatanisho wa kisarufi ; Upatanisho wa kisarufi hutokea kwani
uambatizi huhusika na uambishaji kisarufi. Mofimu za aina moja za umoja na wingi na ambazo
huleta upatanisho wa kisarufi wa namna moja katika vifungu. Hivyo maumbo yote yana
upatanisho wa kisarufi. Mfano;
Umoja wingi alomofu
m-toto wa-toto m- wa-
ki-ti vi-ti ki- vi-
Økaka Økaka Ø- Ø-
Uambatizi wa vitenzi;
Katika uambatizi wa vitenzi upachikaji wa viambishi tangulizi ni vingi kwa mfano katika mzizi
(pig-)
Tu-ta-pig-a
A-li-ye-pig-a Uambatizi hufuata kanuni maalumu kama vile mofimu ya mzizi katika kitenzi
4. Uambatizi wa Vihusishi;
Vihusishi huwa na dhima ya kuunganisha maneno. Mofimu mzizi ya maneno unganishi ni ( a-)
mofimu tangulizi kadhaa huwekwa katika mzizi (-a ) mfano za , ya ,pa, la vinapotumika
katika kuunganisha maneno kama vile pesa za shule, shamba la kaka. Ufanano wa uambatizi na
unyambuzi ninaweza kusema kwamba yote ni matawi ya uambashaji kwa sababu uambatizi na
unyambuzi huhusika na uwekaji na viambishi katika mzizi wa neno kwa kulingana nadhima
mahususi ya kila moja kama ni kubadili kategoria ya neno nakuunda neno jipya au kuleta
upatanisho wa kisarufi.
Utofauti katika maana; Uambatizi ni utaratibu wa uwekaji wa viambishi kwenye mzizi wa
neno ili kulipa neno hilo maana maalamu yaani kupachika viambishi vyenye dhima kisarufi
wataalamu wengine huuita Uambishaji Kisarufi ambapo Unyambuzi ni uwekaji wa viambishi
fuatishi kwenye mzizi wa neno na tokeo lake likiwa ni kubadili maana au kategoria ya
neno.Mifano ya uambatizi ni kama vile;
Wa-na-pig-a ambapo wa- inadokeza nafsi ya tatu wingi pia inadokeza ngeli ya wingi, na-
inadokeza njeo ya wakati uliopo
Uambatizi hufanana kimaana kila kila kiambishi kinapopachikwa ; Kiambishi –m
huweza kuwa na sifa ya ufanano kwani kiambishi hiki huwa ni sehemu ya ngeli moja yaani huwa
katika kundi moja kwa mfano; mke, mto , mtume, mti, mtoto
Hatuorodheshi viambishi kama leksimu, Hii ina maana kwamba mabadiliko ya kisarufi
hatuyaingizi katika kamusi kwa mfano anacheza analima anapika.
Uambatizi haubadili kategoria ya maana ya maneno; viambishi vinavyowekwa
mwanzoni mwa mzizi wa neno hauwezi kubadili kategoria ya maneno kwani maneno huweza
kuandikwa kwa aina mbalimbali japo mzizi wake hubaki kama ulivyo na bado maana ikabaki
kama ilivyo mfano; kitenzi cheza
A-na-chez-a , a-ta-chez-a a-li-chez-a hivyo basi maana ya neno haijabadilika.
Uzalishaji wa vipashio unajitokeza mara nyingi; Katika uambatizi viambishi tangulizi
huwa ni vingi ikilinganishwa na viambishi fuatizi, miifano ya viambishi katika uambatizi ni
kama vile;
Wa-na-o-chez-a, ni-si-ngali-m-pend-a viambishi ni Wa-,na,-o, ni-,si-,ngali-, na m-
Michakato ya unyambuzi vile vile huwa kama ilivyo katika uambatizi utofauti wake upo
kwamba unyambuzi huweza kubadili kategoria
Unyambuzi hujihusisha na mabadiliko ya maana ya leksimu au aina za maneno, kwa
mfano katika utaratibu wa kuunda nomino. Lugha ya Kiswahili huunda nomino nyingi kutokana
na vitenzi, vivumishi.
5. Kwa mfano; Kitenzi Nomino
Lima Kilimo
penda mapendo
Vilevile katika unyambuzi, nomino huweza kubadilika kategoria yake na kwenda katika vitenzi
kwa mfano Nomino vitenzi
Sababu Sababisha
Makini Makinisha
Maneno hufuatwa au kuundwa kwa utaratibu maalumu kwani sio kila kinominishi kinaweza
kutumika kama kinyambuzi mfano tatuwezi kusema kitenzi lima kiwe Kilime
Uzalishaji wa viambishi ni mchache ; katika unyambuzi vipashio vichache
hupatikana ikilinganishwa na viambishi katika uambatizi . mfano wa viambishi vya unyambuzi
Uambatizi unyambuzi
a-li-ye-chez-a m-chez-o
wa-li-o-fund-ish-a ma-fund-ish-o
Kuna mabadiliko kidogo katika viambishi;Katika unyambuzi kuna mabadiliko kidogo
ukilinganisha na uambatizi kwani viambishi huwa ni vya ngeli na kinominishi katika uambatizi
viambishi hufanana kimaana kila kinapopachikwa Viambishi huweza kutofautiana kimaana
viambishi vinapowekwa katika shina au mzizi mfano kiambishi fuatishi cha Kiingereza
Vaporize, Hospitalize Winterize, kuandaa kwa majira ya baridi
Unyambuzi hutokea baada ya mzizi wa neno; mahali ambapo hufanyika unyambuzi au
unyambuaji wa maneno ni baada ya mzizi wa neno lenyewe kwani neno hunyumbuliwa ili
kuzalishwa au kuunda neno jingine jipya.
Unyambuzi huweza kuorodhesha katika kamusi, Katika kamusi maneno
yaliyozalishwa yaani mapya huweza kuwa kama sehemu ya vidahizo katika kamusi kwa mfano
neno Upendo, kilimo, msomi, kisomo, mchezo huweza kuwa kama vidahizo ikilinganishwa na
vitenzi vyake katika uambatizi.
Hivyo ninaweza kuhitimisha kwa kusema kuwa kutokana na mikanganyiko juu ya ipi
ni dhana sahihi ya Uambatizi na Unyambuzi ni vema kuelewa pia dhana halisi ya Uambishaji
kama ilivyojadiliwa katika kazi hii kwani kutokana na uambishaji ndio tunaweza kupata
uambatizi na unyambuzi.
6. MAREJELEO
Massamba D.P.B. na Wenzake (2009) Sarufi Maumbo ya Kiswahili Sanifu
(SAMAKISA) Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Dar se Salaam
Massamba, D.P.B. (2009). Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha. Taaasisi ya
Uchunguzi wa Kiswahili. Dar es salaam.
Kipacha, A(2007) Utangulizi wa Lugha na Isimu Chuo Kikuu Huria Tanzania, Dar-es-
Salaam.
Habwe, J. and Karanja, P (2004) Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi, Phonix
Publishers
Rubanza Y, (1996) Mofolojia ya Kiswahili. Chuo Kikuu Huria
Tanzania, Dar-es- Salaam.