Good Stuff Happens in 1:1 Meetings: Why you need them and how to do them well
Jarida la elimu toleo maalum la maadhimisho wiki ya elimu 2014
1. 1
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
JARIDA LA ELIMU
Toleo la 1/2014 ISSN NO: 1821-8717-1 JUNI, 2014
Maadhimisho ya Wiki ya Elimu
Kitaifa, Dodoma Mei, 2014
Toleo Maalum
2. 2
Wahariri
Mhariri Mkuu
Ntambi Bunyazu
------------
Wahariri Wasaidizi
Elizabeth Pancras
Oliva Kato
------------
Mpiga Picha
Winfrida Lova
-------------
Msanifu
Benjamin Majengo
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
S. L. P. 9121, Dar es salaam
7 Mtaa wa Magogoni, 11479
Simu: +255 2110146,
+255 2110150/2
Tovuti: www.moe.go.tz
Yaliyomo
Tahariri ................................................ 3
Utekelezaji wa BRN katika Sekta
ya Elimu Umeonyesha mafanikio.
Dk. Bilal ..............................................
4
BRN kushirikisha wadau wa elimu
katika utekelezaji wake ...................
6
Serikali Yazindua Mpango wa
kuboresha Elimu ya Msingi nchini ...
7
Programu ya Kukuza Stadi za
Kusoma, Kuandika na Kuhesabu
(LANES); Kuanza Kutekelezwa
Nchini ................................................... 9
Simamieni Vizuri BRN – Pinda ........ 11
Zawadi zilizotolewa katika kilele
cha Maadhimisho ya Wiki
ya Elimu - 2014 ................................. 12
Habari katika Picha 14
3. 3
Tahariri
Kwa mara ya kwanza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa
kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI iliadhimisha Wiki ya
Elimu kuanzia tarehe 3 hadi 10 Mei , 2014. Maadhimisho haya yatakuwa
yakifanyika kila mwaka. Pamoja na malengo mengine, maadhimisho haya
yanalenga kutoa motisha na zawadi kwa shule na wanafunzi waliofanya
vizuri ikiwa ni utekelezaji wa MPANGO WA MATOKEO MAKUBWA SASA
(BRN). Aidha, zawadi pia zilitolewa kwa kila Mkoa na Halmashauri moja
kwa kila Mkoa.
Kupitia maadhimisho haya Serikali na wadau wengine wa elimu walielimisha
umma juu ya umuhimu wa kila mwananchi kuchangia katika juhudi za nchi
yetu kuwa na ELIMU BORA na kuamsha/kuchochea ari ya ushindani wa
kitaaluma kwa wadau mbalimbali wa elimu wakiwemo walimu na wanafunzi.
Maadhimisho ya mwaka huu yalifanyika sambamba na Wiki ya Elimu
Duniani (Global Education Action Week) tarehe 4 Mei hadi 10 Mei, 2014
yakiwa na lengo la kuhamasisha upatikanaji wa elimu kwa watoto wenye
ulemavu.
Malengo ya wiki ya Elimu yalifikiwa kwa vile utoaji wa tuzo kama sehemu
ya motisha kwa shule, walimu na wanafunzi ulifanyika katika sherehe za
maadhimisho ya wiki ya Elimu. Umma wa watanzania ulipata fursa ya
kufahamu programu mbali mbali na ubunifu katika sekta ya Elimu kupitia
maonesho, vipindi maalum katika runinga, redio na magazeti.
Kwa maana hiyo, Maadhimisho ya Wiki ya Elimu Nchini yalionyesha
utekelezaji wa Ilani ya CCM lakini pia kuonyesha utekelezaji wa Mpango wa
Matokeo Makubwa Sasa – Big Results Now (BRN) katika Sekta ya Elimu.
Katika kuadhimisha Wiki ya Elimu, maadhimisho haya yamejumuishwa
pamoja na kuainisha, kuwatambua na kutoa Tuzo kwa Wanafunzi, Walimu,
Shule, Halmashauri na Mikoa iliyofanya vizuri katika Mtihani wa Kumaliza
Elimu ya Msingi na ya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Sekondari Kidato cha
4 mwaka 2013.
Kama inavyosema Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Elimu mwaka huu, Elimu
Bora kwa Kila Mtanzania, Inawezekana Timiza Wajibu Wako, tunatoa
rai kwa Watanzania na wapenda maendeleo ya elimu nchini kushirikiana
na Serikali katika kufanikisha Maadhimisho haya kila mwaka ili kutimiza
malengo ya kutoa motisha kwa walimu na wanafunzi.
4. 4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, amesema kuanza kwa utekelezaji wa
MpangowaMatokeoMakubwaSasakatikaSekta
ya Elimu kumeonyesha mafanikio mbalimbali
katika kuimarisha utoaji wa elimu nchini.
Akizungumza katika Kilele cha Maadhimisho ya
Wiki ya Elimu Tanzania yaliyofanyika kitaifa
katika uwanja wa Jamhuri, mkoani Dodoma Mei,
2014 Dkt. Bilal aliyataja mafanikio hayo kuwa
ni pamoja na Upimaji wa kitaifa wa wanafunzi
wa darasa la II katika uwezo wa kumudu Stadi
za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK)
uliofanyika mwezi Oktoba, 2013. Upimaji huo
ulifanyika katika Halmashauri 20 na ulihusisha
sampuli ya shule 200. Jumla ya wanafunzi 2,264
walifanyiwa upimaji.
“Matokeo ya upimaji huo yatasaidia Serikali
kuandaa programu maalum itakayoliwezesha
Taifa kuondokana na tatizo la wanafunzi
kuendelea na madarasa ya juu bila kuwa na
misingi thabiti ya Kusoma, Kuandika na Kuhesabu
(KKK),” alisema Dkt. Bilal.
Mafanikio mengine ni kuongezeka kwa Ufaulu
wa Elimu ya Msingi na Elimu ya Sekondari kutoka
asilimia 31 na 43 mwaka 2013 hadi kufikia
asilimia 50.6 na asilimia 58.3 mwaka 2014.
Shule za msingi zenye ufaulu wa juu (asilimia
61%-100%) zinazojulikana kama shule za utepe
wa kijani zimeongezeka kutoka 267 mwaka
2012 hadi kufikia shule 616 na zile za Sekondari
kutoka 32 mwaka 2012 hadi shule 146 mwaka
2013.
Asilimia ya Shule zinazojulikana kama shule za
utepe mwekundu zimepungua kutoka 13,669
mwaka 2012 hadi kufikia shule 9,840 mwaka
2013 na zile za sekondari, zimepungua kutoka
shule 3,828 mwaka 2012 hadi kufikia shule 3,592
mwaka 2013. Jitihada ni kuhakikisha kwamba
shule za utepe mwekundu zinapungua kwa kiasi
kikubwa.
Aidha, Serikali katika kutekeleza Mpango wa
Matokeo Makubwa Sasa katika Sekta ya Elimu
imeamndaa na kuweka kwenye tovuti za wizara
(WyEMU - moe.go.tz) na (TAMISEMI - pmoralg.
go.tz) Kiongozi cha Kuimarisha Utendaji wa Shule
chenye madhumuni ya kuwasaidia wakuu wa shule
jinsi ya kusimamia shule kwa ufanisi; Wakuu wa
shule za sekondari zaidi ya 3,000 wamepatiwa
mafunzo ya uongozi na usimamizi wa shule.
“Mafunzo ya uongozi na usimamizi ni muhimu
kwa wale tunaowateua kwa kuwa yatawaezesha
kusimamia vizuri kazi tunazowakabidhi
kuzisimamia, hivyo nawapongeza Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi pamoja OWM –
TAMISEMI kwa kuanzisha na kuendesha mafunzo
haya,”alisema Makamu wa Rais.
Serikali pia imetoa Mafunzo ya kujenga uwezo
wa walimu katika kubaini wanafunzi wenye
mahitaji ya mafunzo na kutoa mafunzo rekebishi
kwa walimu wa shule za sekondari.
Pamoja na mafanikio hayo, zipo changamoto
mbalimbali zinazotokana na upatikanaji wa
rasilimali, hata hivyo Serikali kwa kushirikiana
na wadau mbalimbali imejipanga kukusanya
rasilimalizakutoshailikukabiliananachangamoto
hizo.
Serikali iliamua kubuni mpango wa “Matokeo
Makubwa Sasa” ama kwa Kiingereza “Big Results
Now (BRN)” wenye lengo la kuinua uchumi wa Taifa
kutoka nchi yenye uchumi wa chini hadi uchumi wa
kati ifikapo mwaka 2025 kwa kuimarisha mfumo
wa usimamizi na utendaji kazi ikiwemo utekelezaji
wa miradi ya maendeleo na huduma za jamii
ikiwemo Elimu. Utekelezaji wa mpango wa “Big
Results Now” hapa nchini ulianza kwa kuainisha
maeneo sita ya kipaumbele ili kupata matokeo
makubwa kwa haraka. Maeneo hayo ni Nishati,
Elimu, Maji, Miundombinu, Kilimo na Utafutaji
fedha. Maeneo haya ya kipaumbele yanabeba
msingi wa kufungulia fursa za ukuaji uchumi wa
Tanzania kwa ujumla na kuchochea ustawi wa
maisha bora kwa wananchi. Hatua ya pili, ikawa
ni kufanya uchambuzi wa kina kwa kutumia mtindo
wa maabara katika maeneo sita ya kipaumbele.
IIi kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo ya
Taifa ya Mwaka 2025, ndani ya muda uliobakia
kuanzia mwaka 2011, Serikali iliandaa Mpango
wa Maendeleo wa Muda Mrefu wa Miaka 15
ambao utatekelezwa katika awamu tatu za
miaka mitano mitano. Katika Mpango wa Kwanza
wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/12-
2015/16), maeneo yaliyopewa kipaumbele ni
Miundombinu, Kilimo, Viwanda, Huduma za jamii
na Uendelezaji Rasilimali Watu na Utalii, Biashara
na Huduma za Fedha.
Malengo ya Dira ya Maendeleo ya Taifa ya
Mwaka 2025 ni kuleta maendeleo ya haraka nchini
na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati
ifikapo mwaka 2025. Maana yake ni kwamba
Utekelezaji wa BRN katika Sekta ya Elimu
Umeonyesha Mafanikio – Dk. Bilal
5. 5
wananchi wawe na chakula cha kutosha, huduma ya
elimu na afya iliyo bora iwafikie watu wengi zaidi,
vifo vya watoto na akina mama vipungue, wastani
wa kuishi uongezeke, maji safi na salama yapatikane
kwa wote, uhalifu upungue na umaskini uliokithiri
usiwepo kabisa na pate la wastani la Watanzania
liwe zaidi ya dola za Kimarekani 3,000. Vile vile
pawe na maendeleo ya viwanda, matumizi ya
sayansi na teknolojia yaongezeke, miundombinu
ipanuke na uchumi ukue kwa asilimia 8 na zaidi.
Akizungumzia Maadhimisho ya Wiki ya Elimu nchini,
Dkt. Bilal alisema Maadhimisho hayo yanafanyika
kwa lengo la kuelimisha Umma wa Watanzania juu
ya umuhimu wa Elimu Bora, kuwatambua na kutoa
tuzo kwa wanafunzi, walimu, shule, Halmashauri na
Mikoa iliyofanya vizuri katika Matokeo ya Mtihani
wa Kumaliza Elimu ya Msingi na Sekondari ya Kidato
cha 4 mwaka 2013.
Aidha, kwa kuwatambua na kuwazawadia washindi
hawa, kutachochea ari na kujenga tabia ya ushindani
wa kitaaluma ndani ya mfumo wa Elimu kwa lengo
la kuinua ubora katika ngazi zote za elimu. Vile vile,
kuongeza uwajibikaji katika kufundisha na kujifunza
na hatimaye kuinua ubora wa matokeo ya wanafunzi
ambayo kwa miaka ya hivi karibuni yamekuwa
yakilalamikiwa sana na umma wa Watanzania.
Hivyo, maadhimisho haya yataamsha ari ya wazazi
na jamii kwa ujumla, kushiriki katika shughuli za
maendeleo ya shule na ufuatiliaji wa ufanisi wa
wanafunzi shuleni.
“Jumla ya shule 3,217 zimepata zawadi. Aidha,
zawadi pia zilitolewa kwa kila Mkoa na Halmashauri
moja na Mkoa mmoja, napenda kuwapongeza wote
kwa mafanikio mliyoyapata lakini napenda kuwaasa
pia kupata ushindi ni rahisi kuliko kudumu katika
ushindi. Hivyo, mnayo changamoto ya kufanya bidii
zaidi ili mdumu katika ushindi,” alisema Dkt Bilal.
“Kwa wale ambao hawakupata zawadi, hii ni fursa
nzuri kwao kujifunza kutoka kwa wenzao ama kwa
kufanya ziara za mafunzo katika shule, halmshauri
na mkoa uliofanya vizuri lIi na wao waweze kufanya
vizuri”.
Makamu wa Rais amewataka wazazl/walezi, wadau
wote wa elimu na jamii kwa ujumla kuendelea
kujitolea kwa kuchangia katika masuala ya elimu
ili kuinua ubora wa elimu yetu ambapo aliwataka
kila mmoja kushiriki katika kuweka mikakati thabiti
ya kutekeleza ubunifu na programu mbalimbali
zilizoibuliwa katika Sekta ya Elimu.
Aidha Dkt. Bilal aliishukuru Serikali ya Uingereza kwa
msaada wake wa kuwezesha Mpango wa Kuinua
Ubora wa Elimu Tanzania unaojulika kama Equip -
T. Pia alishukuru Mfuko wa Global Partinership for
Education (GPE) kwa mchango wake wa kusaidia
Mpango wa kuinua kiwango cha umahiri wa
Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK).
Mwanafunzi Dotto Abdallah wa shule ya msingi katika mkoa wa Lindi akisherehesha mbele ya Mgeni Rasmi, Makamu wa Rais
Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal na viongozi wengine katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu kitaifa Dodoma, 2014.
6. 6
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inatekeleza
mpango wa Matokeo Makubwa Sasa kwa kushirikiana
na Wadau wa Maendeleo ili kuinua ubora wa Elimu
nchini. Haya yalisemwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo
ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa katika kilele cha
Maadhimisho ya Wiki ya Elimu yaliyoadhimishwa
mkoani Dodoma katika viwanja vya Jamhuri Kuanzia
tarehe 03-10/05/2014.
Maadhimisho hayo yaliyobeba Kaulimbiu inayosema
“ELIMU BORA KWA WOTE INAWEZEKANA, TIMIZA
WAJIBU WAKO” yaliwakutanisha Washirika wa
Maendeleo, wakazi wa Dodoma na wadau mbalimbali
wa elimu ambapo Maonesho ya Ubunifu na Programu
mbalimbali katika Sekta ya Elimu yalifana.
Dkt. Kawambwa alisema kauli mbiu ya wiki ya elimu
inaweka mkazo kwa wadau wote kubeba jukumu
katika kuinua ubora wa elimu yetu nchini.
Sambamba na hilo Mhe. Kawambwa alisema ikiwa
ni mara ya kwanza Serikali kuadhimisha Wiki ya
Elimu Kitaifa mwaka huu, Maadhimisho haya Kitaifa
yataendelea kufanyika kila Mwaka ambapo pamoja
na mambo mengine yanalenga kuelimisha Umma
wa Watanzania juu ya umuhimu wa Elimu Bora,
kuwatambua na kuwapa tuzo wanafunzi, walimu,
shule, Halmashauri na Mikoa iliyofanya vizuri katika
Matokeo ya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi
na Elimu ya Sekondari (Kidato cha Nne na sita) kila
Mwaka.
Kuhusu utoaji tuzo kwa wanafunzi walimu, shule,
HalmashaurinaMikoailiyofanyavizuriDkt.Kawambwa
alisema ni moja ya mkakati ulioibuliwa katika maabara
kwa kushirikisha wataalamu wa Serikali, Washirika wa
Maendeleo na wadau mbalimbali wa elimu.
Katika kilele cha maadhimisho hayo Makamu wa Rais
Mhe. Dkt. Gharib Bilal alitoa zawadi kwa wanafunzi
ambao walifanya vizuri katika mitihani yao ya
kumaliza elimu ya Msingi na sekondari kidato cha nne
na sita.
Awali wakati maadhimisho hayo yakiendelea Wizara
iliendesha shindano la Uandishi wa Insha ambapo
wanafunzi walioshinda shindano hilo walipewa zawadi
na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru
Kawambwa.
Maadhimisho ya wiki ya elimu pamoja na kufanyika
kitaifa kuanzia tarehe 03 – 10 Mei, 2014, baadhi
ya Mikoa na Halmashauri iliadhimisha Wiki ya Elimu
mapema kwa nyakati tofauti kuanzia mwezi Aprili,
2014. Mikoa hiyo ni Morogoro, Kilimanjaro, Iringa,
Njombe, Mbeya, Geita, Mwanza, Mara, Kigoma,
Ruvuma, Manyara na Kagera. Mikoa mingine 13
imefanya maadhimisho katika Wiki ya Elimu Kitaifa.
BRN Kushirikisha Wadau wa Elimu Katika
Utekelezaji Wake
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa na viongozi wengine wa Elimu wakipata
maelezo kutoka kwa wanafunzi wa shule ya Msingi walioshiriki katika Maonesho ya shughuli mbalimbali za
elimu katika Maadhimisho ya Wiki ya Elimu Mjini Dodoma
7. 7
Uwekezaji mkubwa unaoweka viwango vya juu kuwa
kiini cha utoaji elimu umezinduliwa na Mheshimiwa,
Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 10 Mei
2014 katika Viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma
wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu
Kitaifa. Lengo kuu la Uwekezaji huu ni kuimarisha
mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji kwa watoto
nchini, kama ilivyosisitizwa na Mheshimiwa Rais
aliposema, “Kuboresha elimu ni changamoto yetu
kubwa kwa sasa; changamoto ambayo sisi sote-
serikali, wazazi na jamii - ni lazima tuishughulikie kwa
pamoja”.
Mpango wa Kuinua Ubora wa Elimu Tanzania -
EQUIP -Tanzania – ni mpango wa miaka minne
unaoongozwa na Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI
na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ukiwa na
lengo la kuboresha utoaji wa elimu kwa kuhakikisha
watoto wanapata alama bora kwenye mitihani yao,
na wanaweza kushiriki kikamilifu kutimiza azma ya
kukua na kuchangia kupata maendeleo ya haraka
nchini kwetu Tanzania.
Mpango huu unafadhiliwa na Serikali ya Uingereza
kupitia Shirika la Misaada la Uingereza (DFID -
UKAID), na unafanyakazi katika Wilaya 48, shule
3,700 na utawafikia watoto milioni mbili na laki
moja (2,100,000), malengo yake ni:
Kuboresha utendaji wa walimu kwa kutoa
mafunzo shuleni na motisha ya utendaji kazi
kutaendeleza stadi muhimu za Kusoma, Kusoma
na Kuhesabu (KKK) kwenye shule za msingi
haswa katika madarasa ya awali.
Kuimarisha uongozi na usimamizi wa shule-
Kuwa na mwongozo wa kitaifa wa vigezo
vya shule bora, na kuwaendeleza kitaaluma
Serikali Yazindua Mpango wa kuboresha
Elimu ya Msingi nchini
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa akikata utepe kuzindua banda la
Maonyesho la Equip –T katika Maadhimisho ya Wiki ya Elimu Dodoma, 2014
Inaendelea Uk. 8
8. 8
Walimu Wakuu na Walimu Wakuu Wasaidizi
zaidi ya 7,200 na Waratibu Elimu Kata 755.
Kuimarisha Usimamizi wa Elimu katika ngazi za
Wilaya na Mikoa - Kusaidia menejimenti za
wilaya na mikoa katika Wilaya 48 na Mikoa
7 kuboresha tija na ufanisi wa shule na mifumo
inayowasaidia katika utoaji wa elimu.
Kupanua ushiriki wa jamii - Kuzishirikisha asasi
za kiraia ili wazazi waweze kuona ni kwa jinsi
gani shule zao zinafikia malengo, jamii ione
namna gani fedha zinatumika, kuongezeka kwa
uwajibikaji na hitaji la kuzisaidia shule kuinua
viwango vya utendaji.
“EQUIP-Tanzania inafanya kazi katika mikoa saba ya
Tanzania Bara. Kwa mwaka 2014, EQUIP-Tanzania
imeanza kazi katika mikoa mitano ya Dodoma,
Tabora, Kigoma, Shinyanga na Simiyu. Mwaka 2015,
tutaifikia pia mikoa ya Lindi na Mara” anasema James
Ogondiek, Naibu Mratibu wa Taifa, EQUIP-Tanzania.
Ndani ya miezi michache iliyopita, EQUIP-Tanzania
imeshirikiana na Serikali ya Tanzania kufanya mapitio
ya Mwongozo wa Umahiri wa Walimu wenye lengo
la kuongeza ubora wa walimu, imesaidia kuandaa
Viwango vya Ubora wa Shule vinavyotarajiwa katika
kila darasa kote nchini, na pia itasaidia kuimarisha
Sensa ya Shule ya Mwaka, pamoja na viashiria
vya elimu vilivyokubaliwa na uboreshaji wa zana
na taratibu za ukusanyaji wa takwimu; ambavyo
vitatekelezwa katika mikoa saba lengwa kuanzia
mwezi Julai 2014.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akizindua programu ya kuboresha Elimu ya msingi
inayosimamiwa na Equip – T katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu
Inatoka Uk. 7
9. 9
Tanzania na Sweden wametia saini mkataba wa miaka
mitatu (2014/15 had 2016/17) wa makubaliano ya
Utekelezaji wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na
Kuhesabu (Literacy and Numeracy Education Support
Programme for Tanzania, kwa kifupi LANES) ambao
unafadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Elimu (Global
Partnership for Education, kwa kifupi GPE). GPE imetoa
kiasi cha Dola za Marekani milioni 94.8 ambazo ni
sawa na zaidi ya shilingi za Tanzania bilioni 151 kwa
ajili ya utelekezaji wa programu hiyo, kwa kupitia
Ubalozi wa Sweden nchini.
Kuanzishwa kwa Programu hii ni sehemu ya juhudi
za Serikali katika kutekeleza Mkakati wa Matokeo
Makubwa Sasa; maarufu kama “Big Results Now”.
Programu ya LANES inalenga kusaidia utekelezaji wa
mipango ya miaka mitatu ya Elimu ya Msingi, Elimu
nje ya mfumo rasmi na Elimu ya Makuzi kwa Watoto
Wadogo (Early Childhood Development-ECD) ukilenga
katika Kukuza stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu
kwa watoto walio mashuleni na wale wanaopata Elimu
katika vituo vya Elimu nje ya mfumo rasmi. Maeneo
makuu ambayo yatatekelezwa ni:
Kukuza stadi za ufundishaji na ujifunzaji wa1.
stadi za KKK kwa watoto wa umri kati ya
miaka 5 hadi 13. Hii italenga katika utoaji
wa mafunzo kazini kwa walimu wa Darasa la
kwanza hadi la nne kwa kutumia programu
maalumu ya KKK ambayo itaandaliwa na
serikali. Eneo hili pia litalenga utoaji wa vifaa
vya kujifunzia KKK kwa madarasa hayo katika
shule zote nchini. Zoezi la kutambua utayari
wa watoto katika kujifunza KKK kabla ya
kuandikishwa shuleni pia litatekelezwa.
Kutoa mafunzo na kusaidia kuimarisha miundo2.
mbinu ya kukuza uongozi bora, ukaguzi,
matumizi ya takwimu katika kuandaa mipango
ya Elimu hususan ufundishaji wa KKK na
kuimarisha menejimenti ya Elimu.
Kuhamasisha jamii na wazazi ili wajitokeze3.
katika kuchangia uendeshaji wa Elimu na
ujifunzaji wa stadi za KKK kwenye maeneo
yao.
Katika kusaidia kuimarisha stadi za KKK na kujua
ni wapi pa kuanzia, Tanzania kwa kushiriakiana na
shirika la Maendeleo la Marekani (USAID) ilifanya
utafiti wenye lengo la kupata hali halisi ya uelewa
wa KKK kwa watoto wa darasa la pili. Utafiti huo
umeonyesha kwamba kwa miaka mitano ijayo
(2014/15 had 2018/19) Tanzania itatakiwa kutilia
Programu ya Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na
Kuhesabu (LANES); Kuanza Kutekelezwa Nchini
Inaendelea Uk.10
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya Salum na Balozi wa Sweden nchini Lennarth Hjelmaker wakibadilishana
hati za mkataba wa makubaliano wa kugharamia utekelezaji wa kukuza stadi za KKK. Kulia ni Waziri wa Elimu
na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa akishuhudia makabidhiano hayo.
10. 10
mkazo maeneo makuu yafuatayo ili kuongeza idadi
ya watoto wanaozimudu stadi za KKK:
Kusoma kwa ufahamu kwa watoto wa1.
darasa la kwanza na pili:
Watoto wanaosoma kwa kuelewa:a)
Utafiti huo ulionyesha kwamba ni asilimia
nane tu ya watoto wa darasa la pili ambao
waliweza kusoma na kuelewa yale ambayo
waliyasoma. Ili kubadilisha hali hii, Serikali
kupitia Wizara za Elimu na Mafunzo ya Ufundi
na OWM -TAMISEMI, imeweka malengo ya
kuongeza asilimia hiyo nane ya mwaka 2014
hadi asilimia 40 ifikapo mwaka 2019 (malengo
ya miaka mitano). Kwa mwaka 2015 asilimia
hiyo nane inatarajiwa kupanda hadi asilimia
10, ilhali ikiongezeka hadi asilimia 13 ifikapo
mwaka 2016; asilimia 17 kwa mwaka 2017;
asilimia 24 mwaka 2018 na kufikia asilimia 40
mwaka 2019.
Watoto wanaosoma bila kuelewa kabisa:b)
Utafiti huo ulionesha kwamba asilimia 40 ya
watoto wa darasa la pili husoma bila ufahamu.
Ili kubadilisha hali hii, Serikali imeweka
malengo ya kupunguza asilimia hiyo 40 ya
mwaka 2014 hadi asilimia 21 ifikapo mwaka
2019 (malengo ya miaka mitano). Kwa mwaka
2015 asilimia hiyo 40 inatarajiwa kushuka
hadi asilimia 39, ilhali ikishuka hadi asilimia
37 kwa mwaka 2016; asilimia 35 kwa mwaka
2017; asilimia 31 kwa mwaka 2018 na kufikia
asilimia 21 mwaka 2019.
Ufahamu wa Hisabati kwa watoto wa2.
darasa la kwanza na la pili:
Watoto wanaofanya vizuri (wanaopata zaidia)
ya asilimia 80 ya maswali yanayoulizwa):
Utafiti huo ulionesha kwamba ni asilimia nane tu
ya watoto wa darasa la pili ambao waliweza
kufanya kwa ufasaha maswali ya Hesabu za
Kutoa na Utambuzi wa Tarakimu yanayoendana
na umri wao. Ili kubadilisha hali hii, Serikali
kupitia Wizara za Elimu na Mafunzo ya Ufundi
na TAMISEMI, imeweka malengo ya kuongeza
asilimia hiyo 8 ya mwaka 2014 hadi asilimia
40 ifikapo mwaka 2019 (malengo ya miaka
mitano). Kwa mwaka 2015 asilimia hiyo nane
inatarajiwa kupanda hadi asilimia 10, ilhali
ikiongezeka hadi asilimia 13 kwa mwaka
2016; asilimia 17 kwa mwaka 2017; asilimia
24 kwa mwaka 2018 na kufikia asilimia 40
mwaka 2019.
Watoto wanaopata sifuri kwenye Hisabati:b)
Utafiti huo ulionyesha kwamba ni asilimia
43 ya watoto wa darasa la pili wanaopata
sifuri kwenye mazoezi ya Hesabu za Kutoa
yanayoendana na umri wao. Ili kubadilisha
hali hii, Serikali kupitia Wizara za Elimu na
Mafunzo ya Ufundi na TAMISEMI, imeweka
malengo ya kupunguza asilimia hiyo 43 ya
mwaka 2014 hadi asilimia 21 ifikapo mwaka
2019 (malengo ya miaka mitano). Kwa mwaka
2015 asilimia hiyo 43 inatarajiwa kushuka
hadi asilimia 42, ilhali ikishuka hadi asilimia
40 kwa mwaka 2016; asilimia 37 kwa mwaka
2017; hadi asilimia 32 kwa mwaka 2018 na
kufikia asilimia 21 mwaka 2019.
Kwa hesabu za Utambuzi wa Tarakimu asilimia
10 ya watoto ndiyo wanaopata sifuri. Serikali
imeweka malengo ya kupunguza asilimia hiyo
10 ya mwaka 2014 hadi asilimia 5 ifikapo
mwaka 2019 (malengo ya miaka mitano).
Kwa mwaka 2015 asilimia hiyo 10 haitarajiwi
kupungua, huku ikitarajiwa kushuka hadi
asilimia 9 kwa mwaka 2016; asilimia 8 kwa
mwaka 2017; hadi asilimia 6 mwaka 2018 na
kufikia asilimia 5 mwaka 2019.
Ufaulu wa watoto wanaoingia darasa la3.
tano:
Kwa kutumia mfumo wa uendeshaji wa mitihani
ya darasa la nne uliopo sasa, Serikali ina
lengo la kuhakikisha kwamba wanafunzi
wote wanaoingia darasa la tano wanafaulu
mtihani wa darasa la nne. Programu ya LANES
itachangia katika malengo hayo kwa kutoa
mafunzo kwa walimu wawili kutoka katika
kila shule ya msingi ambao wana jukumu la
kufundisha darasa la tatu na nne.
Ufaulu wa watoto wanaoingia darasa la4.
tano kutoka katika vituo:
ProgramuyaLANESitatoamafunzokwawalimu
wote wanaofundisha katika vituo vya Elimu
nje ya mfumo rasmi na vifaa vya kufundishia
KKK katika vituo vyote ambavyo viko zaidi ya
1680, ikiwa ni vituo10 katika kila Halmashauri.
Lengo likiwa ni kuhakikisha kwamba zaidi ya
asilima 85 ya watoto watakaosoma katika
vituo hivyo wanafaulu mitihani ya KKK na hivyo
kuandikishwa katika mashule katika ngazi ya
darasa la tano.
Programu ya LANES itatekelezwa na Serikali kwa
kushirikiananawadaumbalimbalizikiwemoAsasizisizo
za Kiserikali. Ili kuwe na mabadiliko kwenye malengo
hayo makuu ya KKK ambayo ndiyo msingi wa ufanisi
wa LANES, wadau mbali mbali watatakiwa kuchangia
kwenye programu ya KKK itakayotengenezwa na
kusimamiwa na serikali. Programu hiyo ya KKK
itazingatia maeneo makuu yafuatayo:
Maeneo ya kuzingatiwa ili kuwawezesha na•
kujua kama watoto wamepata ufahamu stahiki
wa stadi za KKK;
Maeneo ya kuzingatia ili kuwawezesha na•
kujua kama walimu wamepata stadi stahiki za
ufundishaji wa KKK;
Vifaa stahiki vya kufund• ishia na kujifunzia
KKK;
Mfumo stahiki wa kupima ufahamu wa KKK•
kwa watoto‘ na
Maeneo ya kuzingatia kwenye usimamizi na ukaguzi
wa ufundishaji na ujifunzaji wa KKK.
Inatoka Uk. 9
11. 11
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda amezitaka
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya
Waziri Mkuu –Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) kusimamia vizuri Mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa katika Sekta ya Elimu (BRN - Edu) ili
kuleta ufanisi.
Mheshimiwa Pinda aliyasema hayo Wakati akifungua
Maadhimisho ya Wiki ya Elimu Kitaifa mkoani Dodoma
Mei, 2014 ambapo alisema kuwa fedha za ukarabati
wa majengo zitumike kikamilifu na Wakurugenzi
watakaozembea, wawajibishwe.
Kuanzishwa kwa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa
(BRN) kumeleta ushindani kwa kupanga shule katika
makundi ya ubora wa ufaulu na kutoa Tuzo kwa shule
3,000 zilizofanya vizuri na zilizoonesha kupiga hatua
katika mtihani wa mwaka 2013. Aidha, Mpango huu
umeweza kuinua kiwango cha ufaulu kutoka Asilimia
30.72 mwaka 2012 hadi 50.61 mwaka 2013 kwa
elimu ya msingi na Asilimia 43.08 mwaka 2012 hadi
Asilimia 58.25 mwaka 2013 kwa Elimu ya Sekondari;
Mpangohuupia,umeimarishausimamizinamenejimenti
ya shule kwa kuandaa kitabu cha kiongozi na kutoa
mafunzo kwa Wakuu wa Shule za Sekondari 3,000.
Aidha, chini ya mpango huu, tumeweza kujenga uwezo
wa ufundishaji na ujifunzaji kwa kutoa mitihani ya
majaribio kwa Darasa VI na VII katika Elimu ya Msingi
na Kidato cha IV kwenye Elimu ya Sekondari, na
kusimamia uimarishaji wa miundo mbinu ya Shule 264.
Hadi kufikia tarehe 31 Machi 2014 miundo mbinu kwa
shule 56 kati ya shule 264 ilikuwa imekamilika.
AkizungumziaElimuMtandao(E-Learning),Mheshimiwa
Pinda alisema Serikali pia imefanya juhudi kubwa
kuinua kiwango cha elimu kupitia Elimu Mtandao
(E-Learning) kwa kupanua mpango wa mtandao
(Bridge IT) ili kufikia shule za msingi 300 kutoka Shule
150 ifikapo Desemba, 2014.
Aidha, Waziri Mkuu alisema Serikali imepanga
kupunguza tatizo la uhaba wa Walimu hususan wa
masomo ya Sayansi na Hisabati kwa kutumia mwalimu
mmoja mahiri katika shule kufundisha madarasa
mengi kwa wakati mmoja. Mpango huu umeandaliwa
ili utumie gharama nafuu na utaanza kutumika Julai,
2014.
Katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi
(CCM) kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka
2010, Serikali iliahidi kuchukua hatua za kuboresha,
Simamieni Vizuri BRN – Pinda
Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akipata maelezo kutoka kwa mwanafunzi wa shule ya msingi ya wasioona,
Bwigiri katika maonesho ya shughuli mbalimbali za elimu katika Maadhimisho ya Wiki ya Elimu.
Inaendelea Uk.17
12. 12
Katika kutekeleza BRN, Sekta ya Elimu ilitoa
zawadi katika makundi mbalimbali kama
ifuatavyo:
KUNDI LA KWANZA: ZAWADI YA CHETI
MAALUMU NA TUZO YA DHAHABU.
Katika kundi hili la Kwanza kuna Shule1.
tano za Msingi; moja isiyo ya Serikali na
nne za Serikali; pamoja na shule tano za
Sekondari mbili zisizo za Serikali na tatu
za Serikali zilizofanya vizuri kwa mwaka
2013 ambapo zawadi yao ni Tuzo ya
Dhahabu ya Cheti Maalumu . Shule hizi ni
kama ifuatavyo:
ShulezaMsinginia. Rockenhill(Shinyanga),
Nyamigogo ‘A’ (Kagera), Ukombozi
(Iringa), Boma sidan (Manyara) na
Murugwanza (Kagera).
Shule za Sekondari ni Kaiziregeb.
(Kagera ), Alliance Girls (Mwanza),
Mzumbe (Morogoro), Ilboru (Arusha)
na Kibaha (Pwani).
Katika kundi hili la Kwanza pia kuna Shule2.
tano za Msingi za Serikali, shule tano za
Sekondari; yaani shule tatu za Serikali
na mbili zisizo za Serikali zilizoongeza
ufaulu kwa asilimia kumi na zaidi kwa
kulinganisha matokeo ya mwaka 2012 na
2013. Shule hizi ni kama ifuatavyo:
Shule za Msingi ni Chimika (Mtwara),a.
Kivukoni (Ruvuma), Kasozibakaya
‘B’ (Kagera), Chiwale (Mtwara) na
Njeula (Morogoro).
Shule za Sekondari ni Wiza (Kagera),b.
Mhuze (Simiyu), Kilakala (Morogoro),
Hagafilo (Njombe) na Likonde
Seminary (Ruvuma).
KUNDI LA PILI: WANAFUNZI WALIOFANYA
VIZURI
Katika kundi hili wapo Wanafunzi 30 bora (watano
Zawadi Zilizotolewa Katika Kilele cha
Maadhimisho ya Wiki ya Elimu - 2014
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa akitoa zawadi kwa mmoja wa washindi
wa shindano la insha lililofanyika wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Elimu kitaifa kwa wanafunzi wa shule za
msingi na sekondari katika Manispaa ya Dodoma
13. 13
wasichana na watano wavulana katika kila ngazi)
yaani 10 waliomaliza darasa la saba, 10 wa
Kidato cha Nne na 10 wa Kidato cha Sita ambao
walipewa fedha taslimu kwa utaratibu ufuatao:
Washindi wa Darasa la Saba walipewa shilingi
125,000 (zawadi kutoka Ubarozi wa China), wale
wa Kidato cha Nne walipewa Shilingi 250,000
(zawadi kutoka Ubarozi wa China) na Vocha
za kununulia Vitabu zenye thamani ya shilingi
500,000 na kwa wahitimu wa Kidato cha Sita
walipewa shilingi 500,000.
Majina yao ni kama ifuatavyo:
Darasa la Saba Mwaka 2013
Wasichana nia) Gladness Nobert Mahigila
(Scolastika – Kilimanjaro), Adiana Peter
Kasoga (Kwema modern – Shinyanga),
Alice zuberi Zayumba (Tusiime - Dar es
salaam), Maria Charles Njau (Tusiime -
Dar es salaam) na Jemmy Edwin Ndunguru
(Tusiime - Dar es salaam).
Wavulana nib) Devis Audiface Anaclet
(St.Peter Claver – Kagera), Hussein
Hemed Hussein (Tusiime - Dar es
salaam), Kelvin Charles Maseke (Tusiime
- Dar es salaam), Sylivester Gaudence
Masimbani (Tusiime - Dar es salaam),
Ashrak Ahmed Mbondela (Tusiime - Dar es
salaam) na John Peter Benedict (Manzese
- Dar es salaam).
Kidato Cha Nne Mwaka 2013.
Wasichana ni Joyceline L. Mareallea)
(Canossa - Dar es salaam), Margret
Kakoko (St. Francis – Mbeya), Robina S
Nicholaus (Marian Girls – Pwani), Sarafina
W. Mariki (Marian Girls – Pwani) na Abby
T. Sembuche (Marian Girls – Pwani).
Wavulana ni Nelson R . Anthonyb)
(Kaizerege – Kagera), Emanuel M.
Gregory (Kaizerege – Kagera), Razack
I. Hassan (St Mathews - Pwani) , Hamisi
Msangi (Eagles – Pwani), na Sunday Mrutu
(Anne Marie – Pwani).
Kidato Cha Sita Mwaka 2013
Wasichana ni Lucylight E. Malya (Mariana)
Girls – Pwani), Edna B. Kibango
(Msalato – Dodoma), Sarah S. Kimaryo
(St Mary’s Mazinde juu – Tanga),
Veronica S.Mwamfupe (Marian Girls –
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa zawadi ya cheti kwa mmoja wa
washindi katika maadhimisho ya Wiki ya Elimu
Inaendelea Uk.16
14. 14
HAB
KATIK
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa cheti cha shukrani
kwa mmoja wa washindi wa shule zilizofanya vizuri wakati wa maadhimisho
ya Wiki ya Elimu kitaifa Manispaa ya Dodoma
Wananchi mbalimbali walioshiriki katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya
Elimu kitaifa yaliyofanyika katika Manispaa ya Dodoma
15. 15
BARI
KA PICHA
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa akitoa
zawadi kwa mmoja wa washindi wa shule zilizofanya vizuri kimasomo wakati
wa maadhimisho ya Wiki ya Elimu kitaifa Manispaa ya Dodoma
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa cheti cha shukrani kwa Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Vijana na Michezo Mhe. Juma Nkamia kwa Wizara yake kuchangia kufanikisha Maadhimisho ya
Wiki ya Elimu
16. 16
Pwani) na Beatrice D. Issara (St Mary Goreti - Kilimanjaro)
Wavulana ni Erasmi Inyase (Ilboru – Arusha), Maige R. Majuto (Kisimiri - Arusha),b)
Gasper Sinfrid Mung’ong’o (Feza Boys - Dar es salaam), Gasper J. S.Setus (St James
Sem – Kilimanjaro) na Christopher L. Stanslaus (Mzumbe – Morogoro).
Washindi wa Insha ya Afrika Mashariki
Vile vile katika kundi hili la wanafunzi waliofanya vizuri, wapo Washindi 10 katika uandishi
wa Insha ya nchi za Afrika Mashariki mwaka 2013 ambapo zawadi ni Dola 300 kwa mshindi
wa kwanza, 250 mshindi wa pili, 200 mshindi wa tatu, 150 mshindi wa nne, 120 msindi wa
tano na Dola 50 kwa mshindi wa sita hadi wa kumi. Majina yao ni kama ifuatavyo:
Na. Jina Jinsi Shule Mkoa
1. Peter Robert ME Tushikamane Morogoro
2 Gwamaka Mrisho ME Lutheran Junior Sem. Morogoro
3 Godbless Kayombo ME St Marks Dar- Es- Salaam
4 Nestory Owano ME Lugalo Iringa
5 Hemed Abdala ME Beit El Ras Zanzibar
6 Boaz Mayunga ME Kibaha Pwani
7 Glory Mareale KE Iringa Girls Iringa
8 Hauran M. Haji KE Muyuni Zanzibar
9 Buharije L. Buharije ME Heritage Pwani
10 Safina Mayagila KE Dar Es Salaam Dar- Es Salaam
Washindi wa Insha ya Nchi za SADC
Viongozi wa Mkoa wa Ruvuma wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Said Mwambungu wakishangilia Kikombe
baada ya Halmashauri ya Mbinga kuibuka mshindi kwa kupata zawadi nyingi katika Kilele cha Maadhimisho ya
Kilele cha Wiki ya Elimu
Inaendelea Uk.16
Inatoka Uk. 13
17. 17
kuimarisha na kupanua elimu kuanzia ngazi ya
Elimu ya Awali hadi Chuo Kikuu. Aidha, imeahidi
kuhakikisha kuwa, Elimu ya Ngazi zote itakayotolewa
Nchini inakuwa elimu bora itakayowezesha vijana
wetu kupata ajira katika Nchi za Jumuiya ya Afrika
ya Mashariki na Duniani kote kwa ujumla.
Maadhimisho ya Wiki ya Elimu Nchini ni moja ya
utekelezaji wa Ilani ya CCM lakini pia ni sehemu ya
Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa – Big Results
Now (BRN) katika Sekta ya Elimu ambayo yanafanyika
kwa mara ya kwanza hapa Nchini. Maadhimisho haya
pia yana lengo la kuelimisha Umma wa Watanzania
juu ya umuhimu wa Elimu Bora na ushiriki wao katika
kuhakikisha kuwa elimu bora inapatikana kwa wote.
Aidha, katika kuadhimisha Wiki ya Elimu, maadhimisho
haya yamejumuishwa pamoja na kuainisha,
kuwatambua na kutoa Tuzo kwa Wanafunzi, Walimu,
Shule, Halmashauri na Mikoa iliyofanya vizuri katika
Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi na ya Mtihani
wa Kumaliza Elimu ya Sekondari Kidato cha 4 mwaka
2013.
Akizungumzia Mwenendo wa Ufaulu wa Mwaka 2013,
Waziri Mkuu alisema taarifa za Matokeo ya Mtihani
wa Kidato cha Nne zinaonesha kuwa, ufaulu wa juu
(Daraja la I-III) kwa mwaka 2013 unaonekana kuwa
mkubwa ukilinganishwa na miaka ya 2010, 2011,
na 2012 kwa shule za Wananchi, Serikali, Binafsi
na Seminari. Aidha, idadi ya watahiniwa waliofaulu
katika madaraja hayo nayo iliongezeka kwa aina zote
za shule. Kwa hali hiyo, ufaulu wa Daraja IV ulishuka
kutokana na kupanda kwa ufaulu katika Madaraja
hayo ya I - III.
Kwa upande wa Shule za Wananchi, Takwimu
zinaonesha kuwa wastani wa ufaulu wa Shule za
Wananchi ni mdogo (Asilimia 48) ikilinganishwa na
Asilimia 59.7 Shule za Serikali; Asilimia 84.3 Shule
Binafsi na Asilimia 80.8 Shule za Seminari. Hata
hivyo, kwa idadi Wanafunzi wengi waliofaulu katika
MitihanihiyoniwakutokakatikaShulezaWananchi
ambao ni 109,229 ikilinganishwa na 52,242 wa
Shule za Binafsi, 33,533 wa Shule za Serikali
na 6,149 wa Shule za Seminari. Hii inatokana
na ukweli kuwa idadi kubwa ya Wanafunzi iko
kwenye Shule za Wananchi.
Aidha, takwimu zinaonesha kuwa, ufaulu
usioridhisha wa Daraja la Sifuri (0) wa Shule za
Wananchi kwa mwaka 2013 ni wa chini kuliko
miaka mitatu iliyopita. Kwa mfano, ufauli wa
Daraja hilo mwaka 2013 ulikuwa Asilimia 51.80,
mwaka 2012 ulikuwa Asilimia 56.93, mwaka 2011
ulikuwa Asilimia 57.46 na mwaka 2010 Asilimia
64.60. Kupungua kwa ufaulu huo kumechangiwa
na kuongezeka kwa ufaulu wa shule hizo kwenye
Daraja la I, II, III na IV.
Kwa kuangalia ufaulu kimasomo, takwimu
zinaonesha kuwa Shule za Binafsi zimeongoza
kwa ufaulu kwenye masomo ya Civics, History,
Geography, English Language, Kiswahili, Biology,
Commerce na Book-keeping. Katika masomo
hayo baada ya Shule Binafsi, zilifuatia Shule za
Seminari, Shule za Serikali na mwisho Shule za
Wananchi. Vilevile, Shule za Seminari zimeongoza
kwa ufaulu kwenye masomo ya Physics, Chemistry
na Basic Mathematics zikifuatiwa na Shule za
Binafsi, Shule za Serikali na Shule za Wananchi.
Shule za Seminari zimeongoza kwa ufaulu
katika masomo ya Sayansi. Kwa ujumla Shule za
Wananchi zimekuwa na ufaulu mdogo kuliko shule
za wamiliki wengine kwa masomo yote muhimu
katika mwaka 2013.
Kutokana na yaliyojitokeza kwenye matokeo
hayo ya Kidato cha Nne mwaka 2013, ni dhahiri
kwamba, Serikali inahitaji kuongeza uwekezaji
kwenye shule zake za Wananchi na zile za Serikali
kwa kasi zaidi. Aidha, kuna umuhimu mkubwa wa
kuangalia upya uwekezaji kwenye shule za vipaji
maalum ili kufikia malengo tuliyojiwekea wakati
wa kuanzishwa kwa shule hizo. Uwekezaji huo
ulenge zaidi kwenye miundombinu, walimu,
ukaguzi, vitabu, na vitendea kazi.
“Napenda nitumie nafasi hii kusisitiza nia ya
Serikali kuendelea na utaratibu wa kushindanisha
Wanafunzi, Walimu, na shule hizi Kitaifa kwa
kutoa zawadi ili kuinua ari ya ushindani katika
utoaji wa elimu bora. Vilevile, nitumie fursa hii ya
awali kupongeza Wanafunzi na Walimu wa Shule
zote zilizofanya vizuri katika Mikoa na Wilaya
zote Nchini. Serikali imeamua kwamba itaendelea
Inatoka Uk. 11
Inaendelea Uk.18
18. 18
na utaratibu wa kutoa Tuzo na zawadi mbalimbali
kwa shule zote zitakazofanya vizuri katika
Mitihani ya Taifa kama motisha na kutambua
juhudi zao. Vilevile, Serikali itaendelea na Mfumo
wa Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa (BRN)
ambapo Sekta ya Elimu ni moja kati ya Sekta Sita
za Kipaumbele katika kuleta maendeleo ya Nchi”
alisema Mheshimiwa Pinda.
“Niwapongeze wale wote waliofanya vizuri
katika matokeo ya mwaka 2013. Bila shaka
kila Mwanafunzi, Mwalimu na Shule mnajipanga
kuwa na matokeo mazuri zaidi mwaka 2014.
Serikali itawazawadia watakaofanya vizuri kwa
mujibu wa utaratibu utakaowekwa. Naamini wote
mnafahamu kuwa inawezekana kufanya vizuri
zaidi muhimu ni kutimiza wajibu wako (It can be
Done, Play your Part)” alisema Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu alizungumzia pia mafanikio
mbalimbali yaliyopatikana katika Sekta ya Elimu
kwa miaka michache iliyopita ambapo alisema
katika kipindi cha 2009 – 2013 Serikali kwa
kushirikiana na Wahisani, Mashirika ya Dini,
Sekta Binafsi na Wananchi kwa ujumla imepata
mafanikio makubwa katika kuimarisha elimu
katika ngazi ya Elimu ya Awali, Elimu ya Msingi,
Elimu ya Sekondari, Mafunzo ya Ufundi Stadi,
na Elimu ya Juu. Mafanikio hayo, yameainishwa
kama ifuatavyo:-
Elimu ya Awali(a)
Serikali imelenga kuwa na darasa la Elimu ya
Awali katika kila Shule ya Msingi. Katika kipindi
cha 2009-2013, Serikali ilipata mafanikio
yafuatayo:
Uandikishaji wa wanafunzi wa Elimu yai.
Awali iliongezeka kutoka Wanafunzi
896,146 mwaka 2009 hadi Wanafunzi
1,026,466 mwaka 2013.
Idadi ya Walimu waliosomea mafunzo yaii.
elimu ya awali ngazi ya cheti imeongezeka
kutoka Walimu 3,279 mwaka 2009 hadi
6,505 mwaka 2013.
Elimu ya Msingi(b)
Baadhi ya mafanikio ya Serikali katika
kusimamia utoaji wa Elimu ya Msingi Nchini ni
haya yafuatayo:
Idadi ya Walimu walioajiriwai.
imeongezeka kutoka 141,713 mwaka
2009 hadi 187,566 mwaka 2013.
Uwiano wa Mwalimu kwa Mwanafunziii.
umeimarika kutoka uwiano wa 1:54
mwaka 2009 hadi uwiano wa 1:43
mwaka 2013.
Idadi ya shule za msingi imeongezekaiii.
kutoka 15,727 mwaka 2009 hadi 16,343
mwaka 2013.
Elimu ya Sekondari(c)
Katika Elimu ya Sekondari Nchini, Serikali
ilifanya yafuatayo:
Idadi ya Shule za Sekondari iliongezekai.
kutoka 4,154 mwaka 2009 hadi shule
4,528 mwaka 2013.
Uandikishaji wa Wanafunzi wa wa rikaii.
lengwa Kidato cha 1 hadi 4 uliongezeka
kutoka 1,401,559 mwaka 2009 hadi
1,728,534 mwaka 2013.
Uandikishaji wa Wanafunzi wa Kidatoiii.
cha 5 – 6 uliongezeka kutoka 64,843
mwaka 2009 hadi 75,522 mwaka
2013.
Uandikishaji wa Wanafunzi wa Kidatoiv.
cha 1 – 6 uliongezeka kutoka 1,466,402
mwaka 2009 hadi 1,804,056 mwaka
2013.
Idadi ya Walimu imeongezeka kutokav.
33,954 mwaka 2009 hadi 73,407
mwaka 2013
Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi StadI(d)
Katika Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi
Stadi Serikali imepata mafanikio yafuatayo:-
Idadi ya Vyuo vya Elimu ya Ufundii.
imeongezeka kutoka 184 2005/2006
hadi kufikia vyuo 744 mwaka 2013.
Nafasi za mafunzo zimeongezeka kutokaii.
Wanafunzi 78,586 mwaka 2005 hadi
kufikia Wanafunzi 121,348 mwaka
2011.
Ujenzi wa Vyuo (17) vipya umekamilika naiii.
kuongeza uwezo wa kuchukua Wanafunzi
3,560 ambapo Vyuo vya Ufundi Stadi vya
Mikoa ya Lindi, Manyara, Pwani na Chuo
chaTEHAMAKipawavimezinduliwamwaka
2012. Ujenzi wa chuo kipya cha Wilaya
ya Makete (Civil Works) umekamilika kwa
Asilimia 98.
Udahili wa Wanafunzi umeongezekaiv.
Inatoka Uk. 17
Inaendelea Uk. 21
19. 19
Vile vile kuna Washindi 3 wa uandishi wa Insha nchi za SADC mwaka 2013 ambapo zawadi ni
Dola 500 kwa mshindi wa kwanza, 300 Mshindi wa pili na 200 mshindi wa tatu. Majina yao
ni kama ifuatavyo:
Na. Jina Jinsi Shule Mkoa
1. Ally Mengi ME Tushikamane Morogoro
2 Emmanuel Wisaka ME Mzumbe Morogoro
3 Kenedy Mlawa ME St. Antony DSM
Halmashauri na Mkoa uliopata zawadi nyingi:Halmshauri ya Mbinga na mkoa wa Tanga
waliongoza kwa kuwa na shule nyingi zilizopata zawadi.
KUNDI LA TATU: TUZO YA SILVER (FEDHA) NA CHETI MAALUMU
Katika kundi la Tatu kuna Shule tano za Msingi; moja isiyo ya Serikali na nne za Serikali; shule tano za
Sekondari mbili zisizo za Serikali na tatu za Serikali zilizofanya vizuri kwa mwaka 2013 ambapo zawadi
yao Cheti Maalumu na Trophies za fedha. Shule hizi ni kama ifuatavyo:
Shule za Msingia.
NA JINA LA SHULE MKOA
1. Tusiime Dar es salaam
2. Nyamigogo ‘B’ Kagera
3. Laalakir Manyara
4. Kagondo ‘B’ Kagera
5 Nyiwa Dar es salaam
Shule za Sekondarib.
NA JINA LA SHULE MKOA
1 Thomas More Machrina Dar es salaam
2 St. Francis girls Mbeya
3 Tabora boys Tabora
4 Kwaludege Tanga
5 Msalato Dodoma
Aidha, katika tuzo hii ya Fedha, na Cheti Maalum kulikuwa na Shule 10 zilizoonesha ongezeko
la ufaulu ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2012 na yale ya mwaka 2013 yaani shule 5 za
Msingi na 5 za Sekondari. Shule hizi ni kama ifuatavyo:
Shule za Msingia)
NA JINA LA SHULE MKOA
1. Murukagati Kagera
2. Makambi Ruvuma
3. Lositete Arusha
4. Mpale Tanga
5 Foroforo Tanga
Shule za Sekondarib)
NA JINA LA SHULE MKOA
1 Maweni Mbeya
2 Kimbe Tanga
3 Mgugu Morogoro
4 Peramiho girls Ruvuma
5 St. Mary goreti Kilimanjaro
Inatoka Uk. 16
20. 20
Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya Salum na Balozi wa Sweden nchini Lennarth Hjelmaker wakisaini hati za mkataba
wa makubaliano wa kugharamia utekelezaji wa kukuza stadi za KKK. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa na Kaimishna wa Elimu Profesa Eustella Bhalalusesa.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akitoa cheti cha shukrani kwa mwakilishi wa kampuni ya
Business Times kwa kuchangia kufanikisha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu
21. 21
kutoka 53,233 mwaka 2005/2006 hadi
kufikia 112,447 mwaka 2011/2012.
Udahili katika Vyuo vya Umma piav.
umeongezeka kutoka Wanafunzi 34,291
mwaka 2005/2006 hadi kufikia 90,641
mwaka 2011/2012.
Udahili wa Wasichana katika Vyuo vyavi.
Elimu ya Ufundi (Vocational Education and
Training) umeongezeka kutoka 35,564
mwaka 2005 hadi 50,190 mwaka 2011.
Elimu ya Juu(e)
Kwa upande wa Elimu ya Juu, yafuatayo
yameweza kufanyika:
Idadi ya Vyuo Vikuu na Vyuo Vikuui.
Vishiriki imeongezeka kutoka vyuo 23
mwaka 2005/2006 hadi 49 mwaka
2012/2013. Vyuo Vikuu 27 na Vyuo
Vikuu Vishiriki 22.
Udahili katika Vyuo Vikuu umeongezekaii.
kutoka Wanafunzi 40,719 mwaka
2005/06 hadi kufikia Wanafunzi
166,484 mwaka 2011/2012.
Ongezeko hili limewezesha ushiriki rika
kwa Elimu ya Juu kuongezeka kutoka
Asilimia 1.27 mwaka 2005/2006
kufikia Asilimia 4 mwaka 2011/2012.
Idadi ya Wanafunzi waliopata mikopoiii.
imeongezeka kutoka Wanafunzi 42,729
mwaka 2005/2006 kufikia Wanafunzi
94,477 mwaka 2011/2012.
Kiwango cha fedha kilichotolewaiv.
na Serikali kwa ajili ya mikopo
kimeongezekakutokaShilingiBilioni56.1
mwaka 2005/2006 hadi kufikia Shilingi
Bilioni 326 mwaka 2012/2013.
Mwaka 2005/2006 utaratibu wav.
kufuatilia walionufaika na mikopo
uliandaliwa. Hadi kufikia mwaka
2011/2012 kiasi cha Shilingi Bilioni
20.1 zimerejeshwa.
Kuanzishwa kwa Mfumo wa udahili wavi.
pamoja wa kujiunga na Vyuo vya Elimu
ya Juu (Central Admission System - CAS).
na
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wavii.
Elimu ya Juu imeanzisha matumizi ya
mtandao katika kuomba mikopo (Online
Loan Application System) ili kuimarisha
mchakato wa utoaji mikopo na utunzaji
wa kumbukumbu za mwombaji mikopo
kuanzia mwaka 2011/2012.
Aidha, Waziri Mkuu alizungumzia pia changamoto
za Sekta ya Elimu ambapo alisema pamoja na
mafanikio, bado kuna changamoto ambazo Serikali
itaendelea kujizatiti kuzisimamia kwa karibu zaidi.
Changamoto hizo ni pamoja na:
Kupandisha kiwango cha ufaulu hususan katika(a)
masomo ya Hisabati, Sayansi na English katika
Shule za Sekondari na Msingi.
Kushughulikia uhaba na uchakavu wa miundo(b)
mbinu katika Shule, Vyuo na Taasisi nyingine za
Elimu.
Kukidhi mahitaji ya Walimu wa sayansi katika(c)
ngazi ya Sekondari na Wahadhiri katika Vyuo
Vikuu;
Kuimarisha upatikanaji wa vifaa vya kutosha(d)
vya kufundishia na kujifunzia, hususan vitabu vya
kiada na vifaa vya maabara na karakana;
Kupunguza idadi ya watu wasiojua Kusoma,(e)
Kuandika na Kuhesabu (KKK);
Kuongeza fursa za Elimu ya Ufundi na Mafunzo(f)
ya Ufundi Stadi;
Kuimarisha miundombinu ya Shule na Vyuo; na(g)
Kuweka mazingira rafiki kwa ajili ya Wanafunzi,(h)
Walimu, Wakufunzi na Wahadhiri wenye
mahitaji maalum.
Upungufu wa madawati katika shule za msingi.(i)
Takwimu zinaonyesha kwamba mahitaji ya
madawati ni 3,302,678; yaliyopo ni 1,837,783
kwa hiyo kuna upungufu wa madawati
1,464,895.
Ili kupunguza tatizo la upungufu wa madawati katika
shule za msingi, Waziri Mkuu aliseama ni lazima hatua
madhubuti zichukuliwe kumaliza tatizo hili haraka
ambpoa aliitaka Wizara ya Elimu kuweka kipaumbele
ili kupunguza tatizo la madawati katika muda mfupi.
Aidha, Mheshimiwa Pinda aliitaka TAMISEMI kuandaa
utaratibu wa kuondoa tatizo la upungufu wa madawati
katika shule za msingi ambapo kila Halmashauri kwa
nafasi yake iwe ya mjini au ya vijijini ina uwezo wa
kupunguza tatizo kulingana na fursa ilizonazo.
Inatoka Uk. 18
22. 22
Picha Juu na Chini: Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa na viongozi wengine
wa Elimu wakipata maelezo toka kwa wanafunzi katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Elimu
23. 23
KUNDI LA NNE: FEDHA TASLIMU
Kwa kutambua kuwa mafanikio ya Shule zetu na pia vijana wetu waliopata zawadi yasingewezekana
kupatikana pasipo juhudi ya pamoja ya Walimu na Uongozi wa Shule kwa ujumla, Shule za Serikali 60 (46
za Msingi na 14 za Sekondari) zilizoonesha ongezeko la ufaulu mwaka 2013 ikilinganishwa na mwaka 2012
zilipewa zawadi ya Shilingi 3,000,000 kila moja kwa ajili ya Walimu waliochangia ufaulu huo. Majina ya Shule
hizo ni kama ifuatavyo:
Shule za Msingi
No. Jina la Shule Mkoa
1 Chimika Primary School Mtwara
2 Kivukoni Primary School Ruvuma
3 Kasozibakaya ‘B’ Primary School Kagera
4 Chiwale Primary School Mtwara
5 Njeula Primary School Morogoro
6 Murukagati Primary School Kagera
7 Makambi Primary School Ruvuma
8 Lositete Primary School Arusha
9 Mpale Primary School Tanga
10 Foroforo Primary School Tanga
11 Bulunga Primary School Mwanza
12 Mnyanza Primary School Morogoro
13 Mali Primary School Tanga
14 Kwendoghoi Primary School Tanga
15 Manza Primary School Morogoro
16 Gwenzaza Primary School Kagera
17 Bwila Primary School Morogoro
18 Monic Primary School Arusha
19 Mgudeni Primary School Morogoro
20 Kimokouwa Primary School Arusha
21 Mikore Primary School Kagera
22 Mfuluni Primary School Morogoro
23 Izyaniche Primary School Mbeya
24 Mnongodi Primary School Mtwara
25 Ntila Primary School Lindi
26 Kibaoni Primary School Lindi
27 Bokwa Primary School Tanga
28 Bunywambele Primary School Kagera
29 Kwampunda Primary School Tanga
30 Ngeta Pwani
31 Rubanga Primary School Kagera
32 Lunyele Primary School Ruvuma
33 Chagana Primary School Tabora
34 Miwaleni Primary School Kilimanjaro
35 Pinde Primary School Morogoro
36 Ilera Primary School Manyara
37 Kulazu Primary School Mwanza
38 Kwamfyomi Primary School Tanga
39 Meserani Primary School Kilimanjaro
40 Lubungo Morogoro
41 Kileguru Tanga
42 Magogoni Morogoro
43 Mwenge Mwanza
44 Kasharazi Kagera
45 Partimbo Manyara
46 Lipuyu Lindi
24. 24
Shule za Sekondari
No. Jina la Shule Mkoa
1 Wiza Secondary School Mbeya
2 Mhunze Secondary School Simiyu
3 Kilakala Secondary School Morogoro
4 Maweni Secondary School Mbeya
5 Kimbe Secondary School Tanga
6 Mgugu Secondary School Morogoro
7 Kwaludege Secondary School Tanga
8 Ilboru Secondary School Arusha
9 Tabora Boys Secondary School Tabora
10 Mwamanenge Secondary School Simiyu
11 Msalato Secondary School Dodoma
12 Kiloleli Secondary School Shinyanga
13 Moshi Secondary School Kilimanjaro
14 Tabora Girls Secondary School Tabora
KUNDI LA TANO: TUZO YA BRONZE NA CHETI.
Kundi la Tano ni la Shule 200; Msingi 100 na Sekondari 100 zenye ufaulu wa juu na zilizoonesha ongezeko la
ufaulu ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2012 na 2013. Katika kundi hili shule zilipokea tuzo ya Bronze na
Cheti, shule hizo ni kama ifuatavyo:
Shule za Msingia)
NA JINA LA SHULE HALMASHAURI MKOA
1 Mahawa independent Eng medium Mwanza jiji Mwanza
2 Boma Kibondo Kigoma
3 Buhembe Bukoba (M) Kagera
4 Sirajul munir Bagamoyo Pwani
5 Mwadui ‘A’ Kishapu Shinyanga
Shule za Sekondarib)
NA JINA LA SHULE HALMASHAURI MKOA
1 Msolwa Kilosa Morogoro
2 Itaga seminary Tabora (M) Tabora
3 Chief wanzagi Musoma (M) Mara
4 Huruma girls Dodoma (M) Dodoma
5 Palloti girls Singida (M) Singida
Shule Zenye Maendeleo Makubwa Kwa Kulinganisha Matokeo Ya Mwaka 2012 Na1.
Mwaka 2013 (Most Improved)
Shule za Msingia)
NA JINA LA SHULE HALMASHAURI MKOA
1. Miesi MASASI MTWARA
2 Ndea MWANGA KILIMANJARO
3 Bulunga SENGEREMA MWANZA
4 Mnyanza MVOMERO MOROGORO
5 Kwendoghoi LUSHOTO TANGA
25. 25
Shule za Sekondarib)
NA JINA LA SHULE HALMASHAURI MKOA
1. Symbiosis NJOMBE (M) NJOMBE
2 Magulilwa IRINGA (V) IRINGA
3 Maghabe MBEYA (V) MBEYA
4 Central Valley ILEMELA MWANZA
5 Wazo Hill KINONDONI DAR ES SALAAM
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal na viongozi wengine wakati wa uzinduzi wa Programu za
kuimarisha Elimu nchini (Equip - T na LANES) wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu
26. 26
ORODHA YA SHULE 180
Orodha ya Shule 90 za Msingia.
Na Jina la Shule Mkoa
1 Mugini Eng Med Pr. School Mwanza
2 Kwema Modern Shinyanga
3 St Magret Pr. School Arusha
4 Tengeru English Medium Pr. School Arusha
5 Prince English Medium Pr. School Kagera
6 Kaizirege Pr. School Kagera
7 Bariadi Alliance Eng Med School Simiyu
8 Lupa English Medium Pr. School Morogoro
9 Rweikiza Pr. School Kagera
10 Imani Pr. School Kilimanjaro
11 Karume Pr. School Kagera
12 Mwanga English Medium Kagera
13 Alliance English Medium Mwanza
14 Kido Pr. School Kagera
15 Rhec English M Pr. School Kagera
16 Qudus Islamic Kagera
17 Mahawa Independent Eng Medium Mwanza
18 Rocken Hill Junior Shinyanga
19 Mwadui Anglican Pr. School Shinyanga
20 Palikas Pr. School Shinyanga
21 Peacland English Medium School Mwanza
22 St Peter Claver Pr. School Kagera
23 Mt Bakita Pr. School Njombe
24 Imani Pr. School Arusha
25 Lumo Pr. School Arusha
26 Twibhoki Pr. School Mara
27 Adolph Kolping Kagera
28 Waja Springs Geita
29 St Achileus Kiwanuka English Medium Kagera
30 Montfort Pr. School Dar Es Salaam
31 Jkibira Eng Medium Pr. School Kagera
32 Ummusalama Pr. School Iringa
33 Kadama English Medium Pr. School Geita
34 Tumaini Junior School Arusha
35 Scolastica Pr. School Kilimanjaro
36 Tegemeo Pr. School Kagera
37 Amani Pr. School Kagera
38 Nalopa Pr. School Arusha
39 Stjoseph’Smilleniumprschool Dar Es Salaam
40 Stjoseph-Rutabo English Medium Kagera
41 Golden Valley Pr. School Geita
42 Maria Magreth Pr. School Kilimanjaro
43 Giti English Medium Pr. School Kilimanjaro
44 Maasai Pr. School Singida
45 Usambara Pre & Ps Tanga
46 Fountain Of Joy Pr. School Dar Es Salaam
47 Lumala Pr. School Mwanza
48 Martin Luther Pr. School Dodoma
49 Mzigu English Medium Mwanza
50 Busara Eng Med Pr. School Mwanza
51 Usagara English Medium Pr. School Mwanza
52 Hazina Pr. School Dar Es Salaam
53 Jelly’S Pr. School Mwanza
54 St Benedict Pr. School Njombe
55 Nyiwa Pr. School Dar Es Salaam
56 Happy Pr. School Kagera
57 Ritaliza Of Mt Carmel Pr. School Kilimanjaro
58 Honest Pr. School Pwani
59 Papango English Medium Pr. School Morogoro
60 Ibambula Pr. School Geita
61 Hady Pr. School Arusha
27. 27
Na Jina la Shule Mkoa
62 Emau English Medium Pr. School Geita
63 Imani Pr. School Kagera
64 Mt Hanang English Medium School Manyara
65 Stdominicsavio Pr. School Iringa
66 High Challenge Pr. School Arusha
67 Heritage Pr. School Dar Es Salaam
68 Act Mara Pr. School Mara
69 Lucky Vicent Pr. School Arusha
70 Holy Cross Pr. School Dar Es Salaam
71 Ngara-Mjini Pr. School Kagera
72 Upendo Eng Med Pr. School Mwanza
73 Olympus Pr. School Mara
74 Minzani Pr. School Kagera
75 Eben Ezer Eng- Md Pr School Tanga
76 Marian Pr. School Pwani
77 Buhembe Pr. School Kagera
78 New Ambassador Pr. School Dar Es Salaam
79 Ilasi English Medium Pr. Schoo Mbeya
80 Nelis English Medium Mwanza
81 Anazak Pr. School Dar Es Salaam
82 Sirajul Munir Pr. School Pwani
83 Bohari Pr. School Kagera
84 Mwadui ‘A’ Pr. School Shinyanga
85 Nyanshimba Pr. School Kagera
86 Makole Pr. School Tanga
87 Fort Ikoma Pr. School Mara
88 Green Acres Pr. School Arusha
89 Omukaliro Pr. School Kagera
90 Igwata Pr. School Simiyu
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa akitoa zawadi ya Ngao kwa mmoja wa
viongozi wa shule zilizofanya vizuri kitaaluma katika Wiki ya Elimu
28. 28
Shule 90 za Sekondarib.
S/N CENTRE NAME Region Name
1 Marian Boys’ Secondary School Pwani
2 Feza Girls’ Secondary School Dar Es Salaam
3 Precious Blood Secondary School Arusha
4 Canossa Secondary School Dar Es Salaam
5 Marian Girls Secondary School Pwani
6 Anwarite Girls’ Secondary School Kilimanjaro
7 Mwanza Alliance Secondary School Mwanza
8 Abbey Secondary School Mtwara
9 Rosmini Secondary School Tanga
10 Don Bosco Seminary Iringa
11 St. Mary Goreti Secondary School Kilimanjaro
12 Queen Of Apostles-Ushirombo Seminary Geita
13 St. Mary’S Mazinde Juu Secondary School Tanga
14 St. James Seminary Kilimanjaro
15 Alpha Secondary School Dar Es Salaam
16 Kifungilo Girls Secondary School Tanga
17 St Amedeus Secondary School Kilimanjaro
18 St. Joseph’S Iterambogo Seminary Kigoma
19 Msolwa Secondary School Morogoro
20 Tengeru Boys Secondary School Arusha
21 Jude Secondary School Arusha
22 St. Joseph-Kilocha Seminary Njombe
23 Bethelsabs Girls Secondary School Iringa
24 Peramiho Girls Secondary School Ruvuma
25 Kandoto Sayansi Girls Secondary School Kilimanjaro
26 Uru Seminary Kilimanjaro
27 Makoko Seminary Secondary School Mara
28 St. Mary’S Junior Seminary Pwani
29 St. Mary’S-Ulete Secondary School Iringa
30 Tusiime Secondary School Dar Es Salaam
31 Sanu Seminary Manyara
32 Feza Boys’ Secondary School Dar Es Salaam
33 Nyegezi Seminary Mwanza
34 Eagles Secondary School Pwani
35 Carmel Secondary School Morogoro
36 Amani Girls Secondary School Singida
37 Maua Seminary Kilimanjaro
38 Hellen’S Secondary School Dar Es Salaam
39 Trust Patrick Secondary School Arusha
40 St. Joseph Millenium Secondary School Dar Es Salaam
41 Rubya Seminary Kagera
42 Sengerema Seminary Mwanza
43 St.Carolus Secondary School Singida
44 Ahmes Secondary School Pwani
45 Pandahill Secondary School Mbeya
46 Brookebond Secondary School Iringa
47 Kasita Seminary Morogoro
48 Mafinga Seminary Iringa
49 Uwata Secondary School Mbeya
50 Itaga Seminary Tabora
51 Anderlek Ridges Secondary School Shinyanga
52 Arusha Catholic Seminary Arusha
53 Dung’Unyi Seminary Singida
54 St. Clara Secondary School Kilimanjaro
55 Likonde Seminary Ruvuma
56 Gift Skilful Secondary School Pwani
57 Rising Star Secondary School Dar Es Salaam
58 S.S. Rufino Rinaldo Secondary School Kigoma
59 Chief Wanzagi Secondary School Mara
60 Star Secondary School Arusha
61 Harrison Uwata Girls Secondary School Mbeya
62 Queen Of Family Secondary School Shinyanga
63 Hekima Secondary School Kagera
64 Visitation Girls’ Secondary School Kilimanjaro
29. 29
65 Chanjale Seminary Kilimanjaro
66 Mhongolo Progressive Secondary School Shinyanga
67 Huruma Girls Secondary School Dodoma
68 Kidugala Lutheran Seminary Njombe
69 Barbro-Johansson Secondary School Dar Es Salaam
70 Kaengesa Seminary Rukwa
71 Agape Lutheran J Seminary Kilimanjaro
72 Donbosco-Didia Secondary School Shinyanga
73 Simba Wa Yuda Secondary School Simiyu
74 Namupa Seminary Lindi
75 African Tabata Secondary School Dar Es Salaam
76 Loyola Secondary School Dar Es Salaam
77 Fray Luis Amigo Secondary School Dar Es Salaam
78 St. Luise Mbinga Girls Secondary School Ruvuma
79 Boniconsili Mabamba Girls Secondary School Kigoma
80 Swilla Secondary School Mbeya
81 Scolastica Secondary School Kilimanjaro
82 Kibosho Girls Secondary School Kilimanjaro
83 Notre Dame Secondary School Arusha
84 Bihawana Junior Seminary Dodoma
85 St. Francis De Sales Seminary Morogoro
86 Bendel Memorial Secondary School Kilimanjaro
87 Baobab Secondary School Pwani
88 Palloti Girls Secondary School Singida
89 Soni Seminary Tanga
90 Mwilamvya Secondary School Kigoma
KUNDI LA SITA
Shule 3,297 za Msingi na shule 159 za Sekondari zilizoonesha ongezeko la ufaulu ikilinganishwa na matokeo
ya 2012 na yale 2013 zilipewa vyeti. Orodha ya shule ni kama ifuatavyo.
Na Mkoa Shule za Sekondari Shule za Msingi Jumla
1 ARUSHA 23 130 153
2 DAR ES SALAAM 32 36 68
3 DODOMA 7 129 136
4 GEITA 1 5 6
5 IRINGA 11 48 59
6 KAGERA 11 320 331
7 KATAVI 1 1
8 KIGOMA 10 130 140
9 KILIMANJARO 32 194 226
10 LINDI 2 146 148
11 MANYARA 1 145 146
12 MARA 7 165 172
13 MBEYA 15 111 126
14 MOROGORO 12 251 263
15 MTWARA 3 211 214
16 MWANZA 20 224 244
17 NJOMBE 7 2 9
18 PWANI 15 130 145
19 RUKWA 3 54 57
20 RUVUMA 7 177 184
21 SHINYANGA 11 61 72
22 SIMIYU 3 2 5
23 SINGIDA 7 106 113
24 TABORA 7 144 151
25 TANGA 11 376 387
JUMLA 259 3297 3556
KUNDI LA SABA: TUZO YA VYETI KWA WAREJESHAJI BORA WA MIKOPO YA ELIMU YA
JUU
Warejeshaji wakubwa wa mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu ni Walimu na walipatiwa vyeti vya pongezi
kupitia kwa kwa Makatibu Wakuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI na wa Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Ufundi ambao watumishi hao wapo chini.
30. 30
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
S. L. P. 9121, Dar es salaam
7 Mtaa wa Magogoni, 11479
Simu: +255 2110146,
+255 2110150/2
Tovuti: www.moe.go.tz
Blog: www.elimutanzania2014.blogspot.com
Facebook: www.facebook.com/moe.go.tz